Monday, March 19, 2012

Muamba bado mahtuti


Bado anatibiwa katika kitengo cha wagonjwa mahtuti.
Meneja wa Bolton Wanderers, Owen Coyle, alisema anatumai matokeo yatakuwa mema kwa Fabrice Muamba, huku mchezaji huyo anaendelea kuuguzwa.
Coyle alisema hayo nje ya London Chest Hospital, ambako ndiko Fabrice anakotibiwa baada ya kuzirai wakati Bolton Wanderers wanacheza na Tottenham Hotspur kwenye uwanja wa White Hart Lane saa 12 magharibi.
Imejulikana leo kuwa matabibu wasaidizi hawakuweza kuufanya moyo wa kijana huyo wa umri wa miaka 23, kuanza kupiga tena wenyewe kwa karibu saaa mbili, baada ya kubanwa na moyo.
Bolton Wanderers wakicheza na Tottenham Hotspur kwenye robo fainali ya kombe la FA.
Coyle aliwaambia waandishi wa habari: "Tunatumai atapona"
Muamba alizaliwa Zaire (sasa inajulikana Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo) na alifika England akiwa na umri wa miaka 11.
Mchezaji huyo kabla ya kujiunga na Bolton Wanderers alitokea klabu ya Birmingham mwaka 2008 na amecheza mechi 148 katika klabu yake ya sasa.
Mashabiki wa timu zote mbili walikuwa wakiimba jina la Muamba wakati alipokuwa akitolewa uwanjani kwa machela.
Na Muamba alikumbukwa katika mechi zote zilizochezwa Jumapili.

0 comments:

Post a Comment